Monday 4 July 2016

Choma meli yako sasa

Ndugu msomaji napenda kutumia wasaa huu kuweza kukusalimia kabla sijaanza kukushirikisha niliyonayo leo. Nianze kwa kukusimulia hadithi moja:

Hapo zamani kuna kiongozi wa nchi fulani alienda vitani na jeshi lake katika nchi ya kigeni kwa kutumia usafiri wa meli. Alipofika pwani ya nchi ya adui aliamuru jeshi lake kuchoma meli waliyokwenda nayo. Aliwaambia wapiganaji wake kwamba kwa sasa wana machaguo mawili tu ambayo ni kushinda ile vita na ni lazima washinde ama kufa wote kwani hawawezi kutoka salama huko kwa kutoroka kwani wameshachoma moto meli yao. Wasiposhinda maana yake watauawa ama watakuwa mateka ama washinde vita na warudi nchini kwao salama. Hapo sasa kukawa hakuna jinsi zaidi ya jeshi lake kuwa na dhamira moja tu ya kushinda

Tuesday 12 May 2015

Hizi ndizo kanuni za kuwa na afya njema

Ili uweze kufanya shughuli zako za kila siku ikiwa ni pamoja na shughuli za uzalishaji mali ni lazima uwe na afya njema. Afya ni hali ya kuwa vizuri kimwili, kiakili, kisaikolojia na kiroho pia. Watu wengi huchukulia kuwa watu wanene ndio wenye afya njema na wakati mwingine hudhani kuwa watu wembamba ndio wenye afya. Lakini kiukweli hilo si kweli.  Mtu mwenye afya ni yule mwenye sifa nilizotaja hapo juu.

Kama huna mojawapo kati ya hivi basi hatuwezi kusema kuwa una afya njema. Ukiwa na afya njema utaweza kuishi maisha yenye furaha na amani na pia utaweza kujizalishia kipato chako kwa kila siku iendayo kwa Mungu. Ili uwe na afya njema inakupasa

Friday 10 April 2015

UKIWA NA VITU HIVI VITATU UTAKUWA NA MAISHA BORA


Maisha ni jinsi unavyoyachukulia mwenyewe. Maisha bora unayaandaa mwenyewe. Kuwa na maisha bora na ya furaha kuna vitu ambavyo unatakiwa kuwa navyo. Vitu hivyo huwezi kuletewa na mtu yeyote isipokuwa wewe mwenyewe. Huhitaji pesa, umaarufu ama madaraka ili uwe na maisha bora na furaha. Simaanishi kwamba pesa, madaraka au umaarufu havihitajiki maishani la hasha, namaanisha kuwa kuwa navyo bila kufanya haya ni ngumu kuwa na maisha bora.
Kubadili vitu unavyoweza kubadili
Kubali usikubali kuna vitu ambavyo unaweza kuvifanya ama kuvibadili maishani, hivi vibadili haraka iwezekanavyo. Usisubiri aje mtu mwingine avibadili kwani mara nyingi vyote vipo ndani uwezo wako. Kubadili tabia zako hakuhitaji usaidizi wa profesa wako wa chuo, bosi wako wala mwenyekiti wako wa mtaa. Je huwezi kubadili tabia yako ya uvivu? Huwezi kubadili tabia yako ya ufujaji wa pesa? Huwezi kuamua kuwa na mafanikio? Huwezi kuwa mwekezaji? Bila shaka tabia hizo na nyinginezo nyingi ziko ndani ya uwezo wako na ukiamua kubadili hakika

Monday 30 March 2015

Kanuni za uongozi bora


Uongozi ni kuonyesha njia kwa wengine. Uongozi thabiti huweza kushinda nyakati ngumu katika hii dunia, huku uongozi mbovu ukiitumbukiza jamii katika majanga na majuto. Dunia hii ishawahi kuwa na viongozi bora sana. Je unamkumbuka Abraham Lincoln, Mwl J.K. Nyerere, Sokoine, Mandela na wengi wengineo ambao wamekuwa mfano wa kuigwa vizazi kwa vizazi. Najua kuna wabovu pia ambao unawafahamu kuanzia ulimwengu wa kwanza mpaka wa tatu. Hayati Dr. Myles Munroe aliwahi kusema ‘jeshi la kondoo linaloongozwa na simba ni rahisi kulishinda kundi la simba linaloongozwa na kondoo’. Maana yake

Thursday 19 March 2015

Namna ya kuwa rafiki bora


Katika makala iliyopita tuliona jinsi marafiki walivyo muhimu katika maisha yetu. Hivyo basi leo nimeona ni bora nijaribu kueleza namna ya kuwa rafiki bora. Ili kuwa rafiki bora huna budi;

Wednesday 18 March 2015

Umuhimu wa kuwa na marafiki


Pengine unaweza kujiulliza ni kwaninini nimeamua kuandika kuhusu umuhimu wa marafiki. Lakini mbali na hilo nikuulize una rafiki?  Najua unalijua jibu lako, lakini nisingependa uniambie. Najua kwamba unajua umuhimu wa marafiki ila nimeona nikukumbushe tu. Marafiki ni tunu kubwa tuliyonayo hapa duniani. Marafiki wanaweza kuwa chanzo cha wewe kufanikiwa ama kuporomoka katika nyanja mbalimbali. Kuna aina mbili za marafiki ambazo nitazitaja ni hapa ambazo ni urafiki wa karibu (close friends) na urafiki wa kawaida (acquaintances). Labda nianze na urafiki wa kawaida. Urafiki wa kawaida ni ule ambao mmekutana sehemu kama baa, kwenye michezo, muziki, sherehe au katika siasa na pia kwenye mitandao ya kijamii kama facebook. Urafiki huu hutokana na nyie kuunganishwa na kitu fulani. Mara nyingi urafiki huu ni wa muda tu na unaweza kuisha pale tu ambapo mtapoteza kile kitu kinachowaunganisha (common interest). Lakini aina ya pili ya urafiki ni ule urafiki wa karibu ambao unakuwa karibu na mtu,

Tuesday 17 March 2015

Namna bora ya kupunguza uzito


Tatizo la uzito mkubwa limekuwa kubwa miongoni mwa jamii yetu. Tatizo hili linachangiwa kwa kiasi kikubwa na ulaji mbovu usiozingatia kanuni za afya. Kukubali kwamba una uzito mkubwa ni nusu ya kulitatua tatizo lako. Ili kujua kama una uzito mkubwa ni lazima uchukue kipimo kinachitwa

Thursday 12 March 2015

Makosa 10 ya kuepuka ili upate mafanikio ya kipesa


Pesa ni chombo kinachotumika kupima thamani ya vitu kama huduma na bidhaa. Pesa hutumika kubadilisha bidhaa na huduma mbalimbali. Kupata na kuhifadhi pesa imekuwa ni changamoto kubwa sana. Hivyo basi ili uweze kufanikiwa yakupasa kujifunza kuhusu pesa. Watu wengi waliofanikiwa wamejifunza na kuelewa pesa.
  1.  Matumizi yasizidi mapato
Ili uweze kufanikiwa kimaisha hasa katika suala la pesa, basi yakupasa kutumia pesa chini ya kiwango unachoingiza. Hii itakusaidia kuweka akiba kwa matumizi ya baadae na